Wednesday, April 18, 2012

Matukio Ya Mchakato wa Uchaguzi Wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki Ulivyokuwa Bungeni Mjini Dodoma.

 Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akisoma malezo ya awali kwa waheshimiwa wabunge namna ambavyo uchaguzi huo utakavyoendeshwa na taratibu zitakazofuatwa.

Naibu waziri wa Ujenzi Mhe. Harison Mwakyembe akimuuliza swali mmoja wa wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki.

Mbunge wa Arumeru Mashariki (CHADEMA) Mhe. Joshua Nassari akimuuliza swali mmoja wa wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki.

Mgombea Ubunge wa Afrika Mashariki katika Kundi la Upinzani John Lifa Chipaka wa TADEA akijibu mojawapo ya maswali yalikuwa yanaulizwa na  wabunge wakati wa zoezi la uchaguzi lililofanyika jana Bungeni Dodoma.

Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah akitoa maelezo ya mwisho kwa wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki kabla ya kuanza kwa zoezi la kujinadi Bungeni jana. kulia kwake ni Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge Nd. John Joel.