Maalim Seif Avitembelea Vyombo vya Habari vya Serikali
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Bw. Yussuf Omar Chunda (katikati) akitoa ufafanuzi juu ya shughuli zinazofanywa na Idara hiyo, wakati Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad alipofanya ziara ya kutembelea Idara hiyo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad aliangalia usanifu wa gazeti la Zanzibar leo wakati alipotembelea shirika la magazeti ya Serikali Zanzibar huko Rahaleo ikiwa ni mfululizo wa ziara zake katika taasisi za Serikali.