Friday, August 3, 2012




Havanna,Cuba.






RAIS KIKWETE ATOA KIFUTA JASHO CHA NG’OMBE KWA WANANCHI WA MONDULI.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha (Longido,Monduli na Ngorongoro) kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009. Kulia kwake ni Mbunge wa Jimbo hilo la Monduli,Mh. Edward Lowassa na Kushoto kwake ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa alipowasili katika kijiji cha Makuyuni,Wilayani Monduli kwa ajili ya kuzindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Makuyuni,wilayani Monduli leo wakati alipofika kuzindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

Rais Kikwete akielekea kwenye jukwaa lililoandaliwa kwa ajili ya kuwahutubia wananchi wa Monduli.

 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Makuyuni,wilayani Monduli leo wakati alipofika kuzindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

Rais Kikwete akiwa na viongozi wenzie kwenye meza kuu.

Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Makuyuni,wilayani Monduli mchana wa leo wakati alipofika kuzindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akitoa shukrani kwa Mh. Rais Jakaya Kikwete kwa kuweza kuwakumbuka wananchi wa wilaya ya Monduli.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akigawa Ng'ombe kwa wananchi wa wilaya tatu za mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

Tuesday, June 26, 2012

Yaliyojiri Kweye Ziara Ya Rais Mohamed Abdelaziz Wa Jamhuri Ya Saharawi

Rais Jakaya Kikwete akimpokea mgeni wake,Rais Mohamed Abdelaziz wa Jamhuri ya Saharawi; Ikulu ya Dar es Salaam, jana terehe 25 Juni, 2012.

Rais JK akitoa hotuba fupi kwa mgeni wake.

Hotuba nzuri mheshimiwa..

Rais Abdelaziz naye akitoa hotuba fupi kwa mwenyeji wake.

Rais Kikwete na mgeni wake wakiangalia brass band ya Jeshi la Polisi.

Picha ya ukumbusho.

JK akimsindikiza mgeni wake.

Rais Abdelaziz akiwaaga wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

JK akimuaga Rais Mohamed Abdelaziz.

Wednesday, April 18, 2012

Dkt. Gharib Bilal Afungua Kongamano La Dini La Waislam Na Wakristo Jijijni Dar Es Salaam Leo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini alipowasili kwenye Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam,kwa ajili ya kufungua Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo, lililoanza leo Aprili 18, 2012.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo lililoanza leo Aprili 18, kwenye Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya Viongozi wa dini baada ya kuzindua rasmi Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo katika Hoteli ya White Sands, jijini Dar es Salaam, leo Aprili 18, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya Viongozi wa Dini, baada ya kuzindua rasmi Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo, katika Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam, leo Aprili 18, 2012.

Matukio Ya Mchakato wa Uchaguzi Wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki Ulivyokuwa Bungeni Mjini Dodoma.

 Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akisoma malezo ya awali kwa waheshimiwa wabunge namna ambavyo uchaguzi huo utakavyoendeshwa na taratibu zitakazofuatwa.

Naibu waziri wa Ujenzi Mhe. Harison Mwakyembe akimuuliza swali mmoja wa wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki.

Mbunge wa Arumeru Mashariki (CHADEMA) Mhe. Joshua Nassari akimuuliza swali mmoja wa wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki.

Mgombea Ubunge wa Afrika Mashariki katika Kundi la Upinzani John Lifa Chipaka wa TADEA akijibu mojawapo ya maswali yalikuwa yanaulizwa na  wabunge wakati wa zoezi la uchaguzi lililofanyika jana Bungeni Dodoma.

Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah akitoa maelezo ya mwisho kwa wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki kabla ya kuanza kwa zoezi la kujinadi Bungeni jana. kulia kwake ni Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge Nd. John Joel.

Matukio Mbalimbali Kutoka Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi; Dkt Ali Mohamed Shein amewapongeza wakulima wa zao la karafuu Zanzibar kwa kuweza kuliuzia Shirika la Taifa la Biashara Zanzibar (ZSTC) karafuu kuliko ilivyotarajiwa kwa msimu huu.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar;Said Ali Mbaruok akizungumza na Balozi mdogo wa China aliyeko Zanzibar Bibi Sheen Limun (mwenye fulana nyeusi) kuhusiana na maswala mbalimbali ikiwa ni pamoja na mikakati ya kuisadia Zanzibar.